Friday, November 16, 2012

MTU MMOJA NA WENGINE WAWILI WAJERUHIWA KUFUATIA VURUGU KATI YA MGAMBO WA JIJI LA MWANZA NA WAMACHINGA

Mtu mmoja ameuawa na wengine wawili kujeruhiwa kufuatiaa vurugu zilizotokea leo majira ya saa tano asubuhi katika eneo la barabara ya Pamba karibu na soko kuu la jijini Mwanza katika vurugu baina ya wafanyabiashara wadogo maarufu kama wamachinga na askari wa Halmashauri ya jiji la Mwanza.
Mtu huyo ambaye jina lake kamili halikupatikana badala yake ametambuliwa kwa jina moja tu la Greda.
Taarifa zaidi zinasema kuwa leo mnamo majira ya saa nne na nusu asubuhi askari wa halmashauri ya jiji wakiwa katika maeneo yao ya kazi eneo la Pamba road kwenye stendi ya zamani ya mabasi ya Tanganyika karibu na soko kuu la jiji la Mwanza, wakiwa katika operesheni zao za kawaida za kusafisha jiji walikamata bidhaa zilizokuwa zimepangwa katika maeneo ambayo hayaruhusiwi kisheria wakiwa kwenye eneo hilo mtu mmoja ambaye anadaiwa kuwa ni mmachinga alimrukia mgambo wa jiji shingoni na kumtolea silaha ya jadi aina ya sime kwa nia ya kumdhuru.
.
Baada ya tukio hilo wamachinga waliokuwa eneo la tukio walianza kuwarushia mgambo hao wa jiji mawe ndipo wale mgambo wa jiji katika kujihami wakaanza kurusha risasi hewani kuwatawanya wamachinga hao waliokuwa wakiongezeka kadri kuanza kwa seleka hilo, kwa bahati mbaya moja kati ya risasi hizo zikampiga mpiga debe mmoja upande wa kushoto na kufariki papo hapo.
Machinga mwingine amejeruhiwa kwenye mkono wa kushoto katika kiwiko, naye dereva wa magari ya biashara za kusafirisha mizigo wa gari aina ya Kenta, magari ambayo hupaki katika eneo hilo amejeruhiwa upande wa kushoto kichwani na kukimbizwa hospitali ya rufaa Bugando kwa matibabu.
Mpaka  saa tisa alasiri baadhi ya maduka katikati ya jiji na karibu na eneo la tukio yalikuwa yamefungwa kabisa licha ya amani kurejea, hiyo ni kutokana na wafanyabiashara kuhofia usalama.
.
.

No comments:

Post a Comment

sikiliza ngoma zinazo kamata kwa sasa

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...