Monday, November 19, 2012

NJOMBE; Mvua zasababisha hasara ya Sh41 milioni Njombe






TATHIMINI  ya mali iliyoharibika kutokana na mvua kubwa iliyonyesha ikiambatana na upepo na kusababisha nyumba kadhaa kuanguka huku nyingine zikiezuliwa paa ni zaidi ya Sh41 milioni.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya mji wa Njombe,  George Mkindo alilimbia gazeti hili ofisni kwake kuwa kazi hiyo imekamilika na imebaini kuwa mvua hiyo iliharibu nyumba 178.
“Hasara iliyopatikana kutokana na uharibifu wa mvua hiyo ni zaidi ya Sh41 milioni, ambayo imetokana na uharibifu wa nyumba 178, vyakula pamoja na mazao shambani,” alisema Mkindo.
Alisema kwa kuwa tathmini  imekwishakamilika na thamani ya uharibifu huo kubainika, hivyo ataituma taarifa hiyo katika ofisi ya Waziri Mkuu kitengo cha maafa.
Hata hivyo alitoa wito kwa wananchi wa mitaa na vijiji vilivyokumbwa na maafa hayo kuendelea kusaidiana na waathirika katika shughuli za ukarabati wa nyumba na mahitaji mengine muhimu, wakati wakisubiri msaada kutoka Serikalini.
Katika hatua nyingine, waathirika wa mafuriko hayo wameanza ukarabati wa nyumba zao bila ya kupata msaada wowote kutoka serikalini.
Uchunguzi wa gazeti hili ulishuhudia baadhi ya waathirika hao wakikarabati nyumba zao huku wakiitaka Serikali kuwasaidia kutokana na tukio kutokea bila ya wao kulitegemea na kuharibu mali nyungi zikiwamo nyumba za mashamba.

No comments:

Post a Comment

sikiliza ngoma zinazo kamata kwa sasa

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...