Wednesday, January 2, 2013

MSANII WA BONGO MOVIES JUMA KILOWOKO AFARIKI DUNIA LEO KATIKAHOSPITAL YA MUHIMBILI


Taarifa za uhakika ni kwamba kweli mwigizaji Sajuki amefariki dunia leo asubuhi (jan 2 2013) katika hospitali ya Muhimbili.
Alilazwa hapo kwa wiki mbili ambapo alikua anasubiri kupata urahisi wa kusafiri kurudi India kwenye matibabu ambayo alipangiwa kurudi tena december 2012.
Dinno ambae ni rafiki wa karibu wa Sajuki ameiambia millardayo.com kwamba tatizo kubwa lililomzuia Sajuki kurudi India ni pumzi ambapo walikua wanatafuta ndege yenye huduma ya gesi.
Baada ya kuhangaika sana, dakika za mwisho ndio walikua wamepata ndege ambayo imekubali kutoa huduma ya gesi kwa Sajuki ambapo Shirika la ndege la Emirates ndio lilikua limekubali kutoa huduma hiyo kumsafirisha mpaka India.
Sajuki alikua na tatizo kubwa la kupumua wakati huu ambapo Dinno amethibitisha kwamba upumuaji wake ulikua unabadilika mara kwa mara.
Msiba upo Tabata, Mwenyenzi Mungu amlaze pema Sajuki.

No comments:

Post a Comment

sikiliza ngoma zinazo kamata kwa sasa

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...