Monday, April 1, 2013

BREAKING NEWS !! MAAFA MENGINE KWA TAIFA, WATU 18 WAFARIKI KATIKA MACHIMBO HUKO ARUSHA, TAZAMA PICHA HAPA


Majeruhi aliyeokolewa.
Mwili wa mmojawapo wa marehemu.
 
Wananchi wa eneo hilo wakiwa na simanzi baada ya ajali hiyo.
----------
Watu zaidi ya 18 wanahofiwa kuwa wamepoteza maisha baada ya kufukiwa na kifusi wakiwa ndani ya mgodi wa Morrum huko Moshono jijini Arusha. 

Kwa sasa wanajeshi wanaendelea na zoezi la uokoaji na tayari majeruhi mmoja ameokolewa na miili ya watu watatu. 

Tukio hili linatokea ikiwa ni siku siku tatu baada ya maafa mengine kutokea jijini Dar es Salaam ambapo watu zaidi ya 30 wamepoteza maisha baada ya jengo la ghorofa 16 kuporomoka.

No comments:

Post a Comment

sikiliza ngoma zinazo kamata kwa sasa

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...