Wednesday, April 24, 2013

MAN UNITED ILIVYOTWAA NA KUSHANGILIA UBINGWA WA ENGLAND 2012/2013


 Saluti Jembe Letu: Wachezaji wa Manchester United wakimpongeza mshambuliaji wao Robin van Persie (kushoto) baada ya kufunga moja ya mabao yake matatu, yaliyoipa United ushindi wa 3-0 dhidi ya Aston Villa na kutawazwa mabingwa wapya wa Ligi Kuu ya England, taji lililokuwa likishikiliwa na mahasimu wao Man City.
 Kiduku cha Ushindi na Utamu Wake: Mholanzi, Robin van Persie (katikati), akishangilia kwa staili ya kucheza muziki baada ya kuiwezesha timu yake kushinda dhidi ya Aston Villa na kutwaa jtaji la 20 katika historia ya Man United, ambalo ni la 13 chini ya Mskochi Sir Alex Ferguson.
 Ubingwa wa Uzeeni Mtamu Bana: Beki mkonngwe Rio Ferdinand (kulia), akiongoza ushangiliaji na wachezaji wenzake wakiwa wamejifunika bendera ya Man United
 Duuh, Hawa Watoto Noma Aisee: Alex Ferguson (wa pili kulia) akishangilia na jopo lake la Maofisa wa Benchi la Ufundi na wachezaji wa akiba, mara baada ya filimbi ya mwisho ya mechi dhidi ya Aston Villa.
 Furaha ya Nahodha Mfaransa: Beki wa kimataifa wa Ufaransa anayeiongoza Man United kwa sasa, Patrice Evra, akishangilia huku akiwa amejifunga bendera ya timu yake kichani.
 Pozi la Picha na Shujaa wa Msimu: Ferdinand, akiwa na nyota wengine wakipozi kwa picha na Robin van Persie aliyeibuka shujaa wa msimu wa klabu hiyo, ambapo jana alifunga mabao yote matatu 'hat-trick.'
 Utu Uzima Dawa: Yoso Mbrazil wa Man United, Rafel da Silva (kushoto) akipiga picha na beki mkongwe wa klabu hiyo, Rio Ferdinand.
 Bao la Kwanza Nalifunga kama Ifuatavyo: Van Persie (kushoto) akipiga shuti kufunga bao la kwanza katika mechi hiyo iliyowapa ubingwa wa Ligi Kuu.
 Fundi Kazini: Van Persie akipokea na kupiga kufunga bao la pili la Man United dhidi ya Aston Villa.
 Huwezi Kuzuia Mvua Weweee!! Van Persie hapa anaonekana akimaliza kazi kwa kufunga bao la tatu la United.
 Sisi Ndio Sisi, Wengine Mafisi: Wachezaji wa Man United wakishangilia ubingwa wa Ligi Kuu.
 Jezi ya Mtaalam Wenu Hii Hapa: Van Persie akionesha jezi yake, ambayo pia inawakilisha idadi ya vikombe vya Ligi Kuu vilivyobebwa na Man United.
 Shampeni ya Ushindi Hiyoooo!! Rio Ferdinand akitingisha na kuwamwagia wenzake shampeni ya kusherehekea ubingwa wa Ligi Kuu.
 Nina Furaha Kuliko Nyie Wote: Ferdinand akiruka juu kwa furaha wakati wa zoezi la kufungua shampeni ya kushangilia ubingwa.
 Hii Yangu Pekee: Ferguson akifungua shampeni yake ya kusherehekea ubingwa na kisha kuanza kuinywa kama anavyoonekana katika picha ya chini.

No comments:

Post a Comment

sikiliza ngoma zinazo kamata kwa sasa

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...