Tuesday, August 27, 2013

RAIS KIKWETE NA MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA MPYA JAJI FRANCIS MUTUNGI NA MSTAAFU MHE JOHN TENDWA

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Msajili wa Vyama vya Siasa Mstaafu Jaji Francis Mutungi na Msajili wa Vyama vya Siasa Mstaafu Mhe John Tendwa baada ya kumuapisha Jaji Mutungi Ikulu jijini Dar es Salaam .

MALI ZA VIGOGO WAUZA "UNGA" ZAKAMATWA, MAJINA 111 YA MAPAPA AU MAPUNDA YATAJWA BADO MANYANGUMI.

VIGOGO 111 wanaosadikiwa kujihusisha na biashara yharamu ya madawa ya kulevya nchini wameanza kuonja 'joto ya jiwe' kufuatia Jeshi la Polisi Tanzania Kitengo cha Kudhibiti na Kupambana na Madawa ya Kulevya kwa kushirikiana na vyombo vingine vya dola kukamata mali zao, Uwazi lina mpango mzima.
Kwa mujibu wa vyanzo makini ndani ya jeshi hilo, pia vigogo wengi wanaojihusisha na biashara hiyo  walikamatwa na kiasi kikubwa cha ‘unga’ ndani ya kipindi cha miaka minne iliyopita.
Kuhusu mali ambazo ni magari, ilidaiwa kuwa kufuatia taarifa zilizowataja wauza unga, jeshi la polisi liliamua kushikilia magari hayo na kufanya uchunguzi wa uhalali wake.
“Kuna watu walitajwa majina, wakafuatiliwa, magari yao yakakamatwa na kufanyiwa uchunguzi, lakini cha kushangaza baadhi yao  wameingia mitini na kutelekeza magari yao,” kilisema chanzo.
Chanzo kilisema baadhi ya magari hayo ni Mercedes Benz, Jeep, Toyota Spacio, Toyota Galsira, Toyota Mark II, Nissan Patrol 4x4 GL, Toyota Land Cruiser na Toyota Prado.   
Uwazi lilifanikiwa kunasa majina ya vigogo waliokamatwa wakiwa na unga  na kiasi walichokamatwa nacho.
Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili katika mahakama mbalimbali nchini na ndani ya jeshi la polisi umebaini kuwa, kesi za watuhumiwa hao zinaendelea kuunguruma kortini  japokuwa kasi yake si ya kuridhisha.

POLISI WABUNI MBINU MPYA
Vyanzo hivyo viliendelea kudai kwamba polisi wamebuni mbinu mpya ya kuwakamata vigogo wa madawa ya kulevya wakiamini itawapa mafanikio zaidi.
“Siku hizi si kama zamani, jeshi la polisi tumebuni mbinu mpya ya kuwakamata hawa jamaa (vigogo). Mbinu hii italeta mafanikio makubwa zaidi,” alisema mtoa habari wetu.

WAPAMBANAJI WA UNGA HATARINI
Taarifa zaidi zinadai kwamba usalama wa viongozi wanaopambana na wahusika wa unga nchini upo shakani kutokana na vitisho vinavyotolewa na mtandao huo duniani kote.
Inaaminika kuwa wengi wanaopambana au kupiga vita madawa ya kulevya, hususan viongozi na waandishi wa habari, hutendwa vibaya wakati mwingine kuuawa kabisa.

UWAZI LAMSAKA KAMANDA NZOWA
Kufuatia taarifa hizo za kiuchunguzi, katikati ya wiki iliyopita, mapaparazi wetu walimtafuta Kamanda wa Kudhibiti na Kupambana na Madawa ya Kulevya Tanzania, Godfrey Nzowa na kumuuliza kuhusu zoezi zima la kamatakamata ya wanamtandao hao.
Kamanda Nzowa alisema zoezi la kuwakamata wanaojihusisha na biashara hiyo linaendelea vizuri.
Alisema mpaka Mei, mwaka huu kikosi chake kimeshakamata kiasi kikubwa cha unga na kuongeza kuwa anaamini kasi ya biashara hiyo nchini imepungua sana.
Aliongeza kuwa askari wake wamejipanga vizuri na wana mafunzo maalum ya kuwatambua watu hao hatari.

VIGOGO HUWALISHA KIAPO KIBAYA  WANAOWABEBESHA
“Tumewakamata ‘mapapa’ (wauza unga wadogo) wengi sana na tunahakikisha kwamba ‘nyangumi’ (wauza unga vigogo)  nao hawachomoki.
“Mara nyingi vigogo wamekuwa wakiwalisha kiapo kibaya vijana wanaowabebesha unga kwamba  ikitokea wakakamatwa wasiwataje lakini nao tunawabana kitaalam mpaka wanawataja, kwa sasa bado tunaendelea kuwadaka,” alisema Kamanda Nzowa.
Kamanda huyo aliwataka wananchi kuendelea kutoa ushirikiano kwa jeshi lake dhidi ya wauza madawa ili kutokomeza kabisa biashara hiyo.

ULINZI VIWANJA VYA NDEGE NCHINI SASA NI MOTO
Katika maongezi yake, Afande Nzowa alisema ulinzi umeimarishwa katika viwanja vya ndege, bandarini, mipaka ya nchi na sehemu zote zinazohisiwa kuweza kupitishwa madawa hayo.

AANIKA MAJINA 111 
Kamanda Nzowa alikwenda mbele zaidi kwa kuweka wazi takwimu ya ukamataji wa watuhumiwa hao kutoka mwaka 2009 hadi Mei, 2013.
Orodha chini inabainisha kiasi na aina ya madawa waliyokamatwa nayo katika mabano.
Steven  Gwaza, (heroin gramu 825.7), Rebecca Wairimu Mwangi (heroin gram 1,800), Khatibu Bakari Khatibu, Khalid Salim Maunga, (cocaine gramu 1,007.4), Dhoulkefly  Awadh, (cocaine gramu 893.58), Abdallah Pashua Kipevu (heroin gramu 31,000), Diaka Brama Kaba (heroin gramu 31,000), huyu alikamatwa akiwa na Ndjane Abubakar, Sylivia Kaaya Namirembe, Farid Kisuule, Robinson Dumba Teise na Ismail Mugabi.


Wengine ni Rashid Salim Mohamed, (cocaine gramu 1,374.32), Mini Thabo Hamza (cocaine gramu 1,595.74), Hamis Mohamed Mtou (cocaine gramu 850), Kwako Sarfo, Mnigeria (cocaine gramu 1,1951.80), Mustapha Musa (cocaine gramu 286), alikuwa na Aman Saidfadhil Daruweshi na Afshin  Jalal.
Kamanda Nzowa akaendelea kuwaanika, Jack Vuyo, (heroin gramu 42,000) huyu alikuwa na Anastazia Elizabeth Cloete. Simon Eugenio Fadu    (cocaine gramu 8,000), Assad  Aziz, (heroin gramu 50,000), alikuwa na Isamil Shebe Ismail, Rashid Salim na Majed Gholamghader.
Wengine kwenye orodha hiyo ni, Anna  Jamaniste Mboya, (cocaine gramu 1,140), Fredy William Chonde (heroin gramu 175,000),  Kambi Zuber, Abdul Ghan na Shahbaz Malik, Livinus Malik (Wapakistani) (cocaine gramu 804.7), Chukwudu  Denis Okechukwu, Paulo Ekechukwu na Hycenth Stan (Wanigeria) (cocaine gramu 81,000).
Aidha wapo, Shoaib S.O. Mohammed, Fedro Alfredo Chongo, (cocaine gramu 1,530), Kadiria  Said Kimaro (heroin gramu 1,365.91),  Abdallah Rajab Mwalimu (cocaine gramu 716.5), Mwiteka Godfrey Mwandemele (cocaine gramu 1,112),  Abbas Kondo Gede (cocaine gramu 1,112), Mwanaidi  Ramadhan Mfundo (cocaiane gramu 5,000), alikuwa na Sarah David Munuo,  Antony  Karanja, Benny Ngare,  Almasi Hamis Said, Yahya Haroun Ibrahim, Aisha Said Kungwi, Rajab Juma Mzome na John  William Mwakalasya.
Wengine ni Ally Mirzai Pirbakhshi (cocaine gramu 97,000) alikuwa na Aziz Juma Kizingiti, Said Mashaka Mrisho, Abdulahman  Mtumwa na Hamidu Kitwana Karimu. 
Ramadhan Athuman (heroin gramu 3,000) alikuwa na Rashid Mohammed, Ally Mohammed Kichaa na Issa Abdulahman. Rashid  Ally Mtopea (heroin gramu 12,000) alikuwa na Idd Adam Mwaduga, Nurdin Adam. Maurine Amatus Lyumba, John  Adams Igwenma  wa (Mnaijeria) ( cocaine gramu 830.19).
Upendo Mohammed Cheusi, Abdallah Omar Salum (cannabis sativa gramu 1,000) alikuwa na Cosmos Chukwumezie, Ifeanyi  Malven Kalu Oko (Wanaijeria)  (heroin gramu 3,185.38), Allan Duller (cocaine gramu 3,882.92), Alberto Mendes kutoka Ghana, (gramu 1,277.10 za heroin)
Wengine ni Joseph Chukwumeka Nwabunwanne Minigeria, (gramu 1,245.96 za heroin) Kwaku Safo Brobbey Mghana (gramu 13,781.78 za heroin), Princewill Ejike Mnigeria (gramu 981.12 za heroin),Mary  Mvula Mzambia (gramu 391.51 za cocaine), Waziri Shaban Mizongi, (gramu 2,013 za heroin) akiwa na Santos Joseph Mpondela, Kelvin Kelven Mwazeni.
Wengine ni Emmanuela Adom, Mghana (gramu 9,838.1 za cocaine), Asha Omary Ramadhan, (gramu 1.56), Mariam Mohammed Said, (gramu 9,857.54 za bangi) akiwa na Abdullatif A. Fundikira
Aliendelea kuwataja Marceline Koivogui, Mghana (gramu 1,073.82 za heroin),  Edwin Cheleh Swen Mliberia (gramu 1,509.35 za heroin),  akiwa na Benjamin Obioma Onuorah  wa Nigeria, Sofia Seif Kingazi, (gramu 3,379.54 za cocaine), Josephine Mumbi Waithera Mkenya (gramu 3,249.82 za cocaine), Iddi Juma Mfaume,( gramu 563.25 za heroine), Amina Kassim Ramadhani,( gramu 1,980.11 za heroine) na Vivian Edigin Mnigeria ( gramu 797.56 za cocaine), Hadija Tambwe,( gramu 33,507.04 Za cannabis),  Sasha Farhan  na Mnyeke Sativa, na Mychel Andriand Takahindangeng Muindonesia,( gramu 3,932.44 za cocaine).
Wengine ni Kristina Biskavevskaja Mluthenia (gramu 4,000 za cocaine), Stephen Basil Ojiofor Mnigeri (gramu 1,173 za cocaine), Judith Marko Kusekwa, ( gramu 1,793 za heroin), Khamis Said Bakari,( gramu 1,793 za heroin).
Kundi la mwisho ni Tabia Omary au Neema Omary (gramu 994.97 za  heroin), Masesa au Habiba Andrew Joseph, ( gramu 1,037.9 za heroin). 
Hivi karibuni Agness Gerald ‘Masogange’ na mwenzake walikamatwa Afrika Kusini wakiwa na kilo 150 za dawa za kulevya.

chanzo:globalpublishers

Monday, August 19, 2013

MSANII LULU AJA NA FOOLISH AGE, KUZINDULIWA MLIMANI CITY MWISHO WA MWEZI HUU..SIO YA KUKOSA HII


Msaani mwenye kipaji cha Hali ya juu nchini na Mwenye umri mdogo Elizabeth Michael "LULU"anatarajia kuzindua filamu yake ya Kwanza tokea alipotoka Gerezani, Filamu hii iitwayo FOOLISH AGE ikiwa imetengezwa na Kampuni ya Proin Promotions Limited itazinduliwa Mnamo tarehe 30 August 2013 Katika Ukumbi wa Mlimani city jijini Dar Es Salaam. 
 
Filamu hiyo inayoelezea Maisha ya kila binadamu katika kila hatua anayopitia katika ukuaji wake.Ni moja ya filamu nzuri na yenye ubora wa hali ya juu kutokana na Sauti,Picha hadi maeneo yaliyotumiwa kucheza filamu.Pamoja na kuwepo lulu humo pia utamuona Msanii Mkongwe Jengua.Filamu hiyo imetengenezwa na Kampuni ya Proin Promotions Limited na Itakuwa ikisambazwa Na Proin Promotions Limited.Katika Uzinduzi huo wa Filamu hiyo ya Lulu Wasanii mbalimbali akiwemo mwanamuziki Lady Jaydee na Machozi Band anatarajiwa kushusha bonge moja la burudani ya kufa mtu.

sikiliza ngoma zinazo kamata kwa sasa

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...