Wednesday, September 11, 2013

BAADA YA SAFARI NDEFU YA KUWANIA NAFASI YA KUFUZU KUCHEZA KOMBE LA DUNIA 2014 HIZI NDIZO ZILIZO FUZU


germany
Safari ya kuelekea kwenye michuano mikubwa kuliko yote katika mchezo wa soka ya Kombe la Dunia la FIFA imeanza kuiva .
Huku michezo ya kufuzu kwa michuano hiyo ikiwa ukingoni ikiwa imesaliwa na raundi mbili za mechi kwa kila kanda tayari kuna mataifa ya meshakata tiketi ya kucheza michuano hiyo baada ya kufuzu mapema huku kukiwa na mechi kadhaa za kufuzu zimebakia .
Barani ulaya mataifa kama Ujerumani , Italia , na Uholanzi zilifanikiwa kukata tiketi baada ya matokeo ya michezo yao ya jana ambapo Ujerumani iliwafunga San Marino 3-0 . Italia walifuzu baada ya kushinda kwa 2-1 dhidi ya jamhuri ya Czech na Uholanzi walikata tiketi yao baada ya kuwafunga Andorra 2-0.
Barani Amerika ya kusini Argentina walifanikiwa kuwa timu ya kwanza kwenye kanda ya CONMEBOL kufuzu baada ya kuwafunga Paraguay 5-2 huku nahodha na nyota wa timu hiyo Lionel Messi akifunga mabao mawili .
Mabao mawili ya Robin Van Persie yalitosha kuwapa Uholanzi tiketi ya kwenda Brazil 2014.
Mabao mawili ya Robin Van Persie yalitosha kuwapa Uholanzi tiketi ya kwenda Brazil 2014.
Italia waliungana na Uholanzi na Ujerumani kama timu za kwanza kufuzu kombe la dunia toka Ulaya.
Italia waliungana na Uholanzi na Ujerumani kama timu za kwanza kufuzu kombe la dunia toka Ulaya.

Amerika ya Kaskazini ilishuhudia timu ya taifa ya Marekani ikifuzu baada ya kuwafunga watani wao wa jadi Mexico 2-0 . Marekani wanaungana na Costa Rica ambao watakuwa wanashiriki kombe la dunia kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2006 baada ya kufuzu kwa matokeo ya sare ya 2-2 katika mchezo dhidi ya Honduras.
Nahodha wa Argentina Messi aliwaongoza wenzie kuelekea Brazil kwenye kombe la dunia.
Nahodha wa Argentina Messi aliwaongoza wenzie kuelekea Brazil kwenye kombe la dunia.
Kabla ya jana timu toka ukanda wa bara la Asia kama Japan , Australia ,Iran na Korea ya Kusini tayari zilikuwa zimefuzu mapema huku mchakato wa kufuzu wa bara hilo ukiisha mapema .
Barani Afrika mchakato wa kufuzu uko kwenye hatua zake za mwisho ambapo timu kumi zimefuzu kwenye hatua ya mtoano itakayohusisha mechi mbili nyumbani na ugenini zitakazotoa timu tano zitakazoiwakilisha Afrika huko Brazil.
Timu za Ethiopia,Cape Verde,Egypt,Algeria,Nigeria , Ghana , Ivory Coast,Cameroo,Senegal na Burkina Faso zitapangiwa mechi mbili ambazo ratiba yake itapangwa jumatatu ijayo .

No comments:

Post a Comment

sikiliza ngoma zinazo kamata kwa sasa

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...