Thursday, December 20, 2012

PATA KUJUA JUU YA TUHUMA KWA ZITTO NA KUNDI LAKE KUTOKA KWA MAMUYA...


Bahati mbaya nimekuja wakati mjadala ukiwa tayari umefungwa na sikuweza kupata fursa ya kujibu baadhi ya hoja ambazo kimsingi zilikuwa zinatakiwa kupewa majibu. Mwanzoni sikutaka kushiriki kabisa mjadala huu lakini baada ya Mhe. Zitto kushiriki imenilazimu walau niseme machache.

Katika thread hiyo - Huyo ndiye Ben Saanane na majibu ya Zitto Mhe. Zitto aliandika hivi:


Quote By Zitto View Post
Ninasikitika sana kuona wanachama wa CHADEMA wanavyoweza kutumika kwa maslahi ya kundi fulani kuharibu heshima ya viongozi wao mbele ya jamii.

Ninaomba ndugu Ben Saanane aje hapa jukwaani kuthibitisha maelezo haya ya Bwana Mamuya kutoka Arusha. Mimi binafsi nikikutana na Ben Saanane leo naweza kupishana naye maana sijawi kumwona, wala kukutana naye. Ndugu Ben Saanane nimewasiliana naye kwenye simu mara mbili au tatu kuhusu masuala yake ya kitaaluma au pale alipohisi kuonewa ndani ya chama. Sijawahi kukutana naye hata siku moja. Kama nasema uwongo yeye binafsi aje hapa kukanusha.

Mimi pamoja na wenzangu tumejenga chama hiki mpaka hapa tulipofika. Tumeingiza watu kwenye chama hiki ili kwa pamoja tuweze kujenga asasi imara kabisa ya kidemokrasia. Chama hiki kina damu yangu. Chama hiki kina muda wangu. Chama hiki kina jasho langu. Nitakuwa mtu wa mwisho kusaliti chama hiki. Sijawahi kuwa mwanachama wa chama chochote cha siasa tofauti na CHADEMA. Sitarajii kuwa mwanachama wa chama zaidi ya CHADEMA.

Ninawasihi wana CHADEMA tuache propaganda za kuchafuana. Nguvu kubwa inayotumika kumchafua Zitto ielekezwe kwenye kujenga taasisi imara ya CHADEMA, chama chenye demokrasia, kisicho na upendeleo, chenye uwakilishi wa kitaifa na chenye kuthamini nafasi ya kila mwanachama.

Mamuya, mara kadhaa umetaka kuniona kwa sbaabu nisizozijua na imekuwa ikishindikana. Unapata dhambi kubwa sana kumwaga sumu unayomwaga kwa mtu usiyemjua wala hujawahi kukutana naye.Acha kutumika. Jisimamie. Simamia chama.

Vijana, wote wa vyama vyote, siku zote simamieni misingi (principles) na sio kusimamia watu. Watu sio mawe. Mtaja juta. Misingi inadumu. Watu hawadumu. Acheni kuramba miguu ya watu. Simamieni misingi ya chama. Misingi ya nchi yetu. Misingi ya demokrasia. Kataeni kutumika.

Angalieni, wanaozungumzia sana usaliti waweza kuta ndio wasaliti wakubwa. wanazungumzia usaliti kama 'defensive mechanism'.

Tuacheni ujinga huu. Tufanye kazi. Kazi tu ndio kipimo cha ukamanda na sio kurambaramba visigino vya watu.

Mwisho, nasikia sikia sana habari za kuchinjana. Kuuana nk. Nasikia habari hizi kwa watu wale wale wa kikundi kile kile. Moja, natoka Kigoma. Nimeaga kwetu. Nitakufa kwa amri ya Mungu. Siogopi kufa. Iwapo kifo changu kitatokana na mkono wa mtu, sidhani kama kwa mtu huyo kama hata panya atabaki nyumbani kwao. Underline this.

Pili, revolutioneries don't talk about deaths. Only cowards do.
Ndugu Zitto na Wanabodi,

Kama nilivyosema awali, sikutaka kuchangia mjadala huo tangu jana kwakuwa niliamini mambo nyeti yaliyopo yataelekezwa kwenye vikao ndani ya Chama.

Ingawa hawezi kuwa sahihi kwa asilimia 100 kwa alichoandika, lakini Exaud Mamuya amekuwa na haraka kidogo kutokana na kushindwa kuvumilia yeye alichoona kama ‘uchafu na hujuma’ vinayoendelea dhidi ya CHADEMA na viongozi wake.

Katika kundi hili alilolitaja Mamuya karibia wote tumeshakaa nao na mara ya kwanza Mamuya alishtuka sana aliposikia kilichokuwa kikijadiliwa kwenye kundi hilo. Pamoja na kushtuka lakini hakushangazwa sana maana hata kwenye sakata la madiwani wa Arusha anajua jinsi Mhe. Zitto alivyohusika na kumuahidi kwamba utamuunga mkono. Tulipotoka kwenye kikao kile alisononeka sana na aliniuliza mambo mengi sana kuhusu kundi hili na mengine nilipanga kuyasema ndani ya vikao hasa yale mambo ambayo ni very very sensitive.

Sasa kwa sababu kiongozi wangu Zitto Kabwe ameibuka na kujaribu kukanusha na kupotosha imebidi nije niweke sawa upotoshaji huu japo kwa kifupi:

Ndugu Zitto,

Mosi:
Sishangazwi na kauli yako kwamba hunifahamu. Ni muendelezo wa siasa zile zile za kutosimamia ukweli na kuendekeza siasa za uongo na upotoshaji. Nimemkumbuka Mwanasiasa Mzee Stephen Wassira (Aliyekitabiria CHADEMA kwamba kitasambaratika) aliposimama na kumkana Mwanafamilia wake mbele ya vyombo vya habari kwa sababu ya siasa na katika mkakati wa kuendeleza ghiliba. Kama mwanasiasa wa Tanzania anaweza kumkana hata mwanafamilia au kusema chochote hakuna la kushangaza.

Sasa, kwa kuwa ushahidi ninao wa jinsi tunavyofahamina na jinsi tulivyoshirikiana kuwashughulikia viongozi wa juu wa chama pamoja na uhusika wetu katika hujuma dhidi ya chama nitaomba chama changu sasa kiitishe kikao cha dharura ili nimwage mambo yote nyeti na ushahidi nilio nao ndani ya vikao. Naamini katika vikao kwa kuwa napenda kuona CHADEMA kikikua kama Taasisi imara ya mabadiliko.

Jana nilimwambia Dr. Kitila haya mambo baada ya wewe kuongea nae na kunitaka mimi niingie JF nikanushe thread hii iliyoanzishwa na Mamuya. Kumbe shinikizo lote ulitaka nikusafishe tu, kitu ambacho sikuwa tayari kufanya. Ushahidi nianao pia! Ulipoona imeshindikana mimi kumkana Exaud Mamuya, wewe ukaamua kuja huku kuja kunikana. Hizo rhetorics unazotumia katika dhana ya kujenga ukabila kwa kufanya ulinganisho wa Mamuya na Ben Saanane ni muendelezo wa propaganda chafu dhidi ya chama ambazo mimi na wewe tulikuwa tukizitumia kuhalalisha kazi yetu hii ambayo kimsingi niliamua kuachana nayo na sikuwa tayari kuendelea kuishiriki.

Pili:

Nigusie kidogo hizi tuhuma za ‘kuuana na kuchinjana’. Tafadhali sana naomba uwe mkweli na usimamie kauli yako ya ‘siasa za ukweli na uwazi’. Hizi siasa za uzandiki hazitufikishi popote. Hizi ni tuhuma ambazo zimekuwa zikisambazwa na kundi la akina ‘TUNTEMEKE’ ambao sote tunawajua yaani mimi na wewe. Hawa tumefanya nao kazi kubwa tangu uchaguzi wa BAVICHA. Madai haya yamekua yakitolewa na Habibu Mchange na Mtela Mwampamba wakishirikiana na Gwakisa baada ya kuona mimi sitaki kushiriki hujuma kwa chama changu.

Wamekuwa wakiandika haya hapa JamiiForums kwamba nimetumwa kukuua. Wamekuwa wakiandika walinikamata na sumu ya kutaka kukuua wewe. Leo unaleta mambo haya hapa! Pia wamekuwa wakinipigia na kunitumia message za kunituhumu kwa haya na kunitisha. Hii ni 'pre-emptive attack'.

Mmekuwa frustrated baada ya kuona jitihada zenu za kunitumia kufikia malengo yenu kwa kutumia mwanya mlioupata baada ya mimi kutoridhishwa na mchakato ule wa BAVICHA zinagonga mwamba. Chama hiki watu wamekifia. Kama kuna damu yako hata mimi na wengine tuna damu yetu hapo pia!

Kazi hii ya kuzusha tuhuma kwa mtu ambaye tunaona anatuvurugia malengo yetu tuliifanya sana na ninaijua kaka! Mmesahau tumekuwa tukifanya jitihada za kumtenganisha mwenyekiti na Katibu mkuu kwanza ili tuweze kuwashinda kwa pamoja? Hili unalijua moyoni mwako . Sasa naomba kama hutanithibitishia tuhuma hizi nitaomba kwa kuwa wewe ni kiongozi wa chama kikao kiitishwe na nitamwaga yote huko. Kama hutafanya hivyo, mimi nitaandika Barua kwa katibu mkuu ili uje unithibitishie tuhuma hizi pamoja na kundi zima la ‘Masalia’. Sitaogopa chochote na nipo tayari kwa lolote kwa kuusema ukweli. Sikutaka kujibu thread hii lakini tuhuma za kutaka kuuana ni serious allegations kwa kuwa zinahusu maisha ya mtu. Kuliko nifanye siasa za aina hii, ni bora niache siasa kaka.

Pia, vitisho vya kuaga kwenu havinihusu na wala havinitishi. Siamini kama ushirikina una nguvu kwangu na hilo unalijua na kundi lote la masalia linajua ndiyo maana ilishindikana mimi kwenda kula viapo kwa mganga wa kienyeji na unakumbuka vizuri! (Ati kula kiapo kwa kundi la masalia ili tusisalitiane katika kazi ya kukihujuma chama chetu). Afadhali Juliana Shonza na rafiki yangu Emmanuel Mwakajila waliniunga mkono katika kukataa hili. Ninaye Mungu anayenipigania na sitaogopa vitisho vyovyote. Mnanifahamu kwa hili, I dare you to challenge me! Twende kwenye vikao.

Mwisho:

WanaJF,
Mambo mengi sitaweza kuyaweka hapa kwa kuwa ni nyeti sana, nitasubiri vikikao ndani ya chama ili kikao kiitishwe nimwage huko. Nadhani safari hii tutakomesha tabia hii chafu ya baadhi ya wanasiasa kujaribu kuwatumia vijana kwa maslahi binafsi. Naamini itakuwa ni kikomo cha siasa za uzandiki na uongo ndani ya vyama vyetu vya siasa.

Wale wanaosema mimi ni mtu wa kutumika, nitapata fursa ya kuwathibitishia hayo. Sinunuliki na sina price tag. Wanaosema haya, ukweli wanaujua moyoni. Ninajiamini kwa kuwa nina taaluma yangu na miradi yangu na sinunuliki labda bei yangu ni Ukweli ambao nipo tayari pia kuulipia in return kwa gharama ya damu yangu.

Brave people, given the opportunity and even under any oppression or threat to life, stay and defend their comrade in arms and their entity....not run away and abandon it....unless something hinders their dignity and pride. Wanamapinduzi wote hufanya haya!

Nyongeza ya Mamuya:
Quote By Exaud Mamuya View Post
Nawasalimu sana ndugu zangu hapa jamvini,

Kwa kweli tokea asubuhi ya leo nimekuwa nikipitia michango mbalimbali ya wana janvi hapa na kuona ni jinsi gani ambavyo njia ya muongo huwa ni fupi.

Kwanza kabisa napenda kumwambia naibu katibu wangu mkuu ya kwamba asifikiri vijana wa miaka hii ni sawa na wale wa mfumo wa chama kimoja kipindi kile! Ameweza kujitutumua kwa kujaribu kujitetea pasipo kujibu hoja ya msingi.

Bwana Zitto Zuberi Kabwe ulichokifanya hapa ni kujaribu kuwaonyesha wana jamvi ya kuwa hatufahamiani na kuonyesha ya kwamba tunatumika na baadhi ya watu flani pasipo kujibu hoja ya msingi ya kwamba WEWE NI MFADHILI WA KIKUNDI CHA WAASI WA CHADEMA!

Bwana Zitto labda nikukumbushe na nadhani utakuwa unakumbuka vizuri siku ambayo tulikuwa wote pale MOUNT MERU HOTEL Arusha pamoja na RUGE wa Clouse Radio, Shyrose Bhanji na baada ya kuachana mlielekea NAURA SPRING HOTEL kwa ajili ya tamasha la miss Arusha na baada ya pale tulipanga kukutana lakini ulipokuja kuniuliza niko wapi nilikwambia niko TRIPLE A Club na ukaniambia umechoka unaenda kupumzika so tuonane kesho yake lakini kesho yake hatukutafutana tena. Sasa unaposema hunifahamu mimi nakushangaa sana kamanda!

Bwana Zitto ikumbukwe vizuri ya kwamba wewe ndo uliyekuwa UKICHOCHEA MGOGORO WA MADIWANI kwa lengo la kumdhoofisha mh Lema kisiasa na mipango na mikakati yote ilikuwa ikifanywa baina yangu mimi, wewe Dr Kitila Mkumbo pamoja na madiwani waliofukuzwa Chadema.

Wewe ndio uliokuwa ukiwapa moyo madiwani wa Chadema kwamba wagome mpaka dakika za mwisho na wasikubali kuomba msamaha hata mbele ya kukao cha ngazi ya juu cha chama yaani KAMATI KUU na hata ulipokuwa ndani ya kikao cha kamati kuu na madiwani wale wapo nje ya ukumbi wa kikao ulikuwa ukiwasiliana nao kwa sms ambazo walinifowardia baadae.

Nilikubali kukusikiliza kama kiongozi wangu wa juu wa chama na kutekeleza yale yote ya usaliti niliyoyafanya na hata ndiyo maana mara nyingi nilikuwa Dar nikikutana na Mchange, Mwampamba, Juliana Shonza, Gwakisa, Festo Sanga kwa ajili ya kupanga mikakati thabiti ya kuwadhoofisha viongozi wakuu wapigania ukweli ndani ya chama sana sana mh Mbowe na Dr Slaa kwa lengo la kuwagombanisha na kupata upenyo wa wewe kuwa juu kisiasa zaidi yao ( divide and rule).

Na hata Dr Kitila mkumbo alikuwa akitupa kila kitu ili kufanyikisha mkakati wa kuwafanya madiwani wa Arusha wawe juu ya mh Lema zaidi zaidi diwani Estomih Mala awe na nguvu kisiasa zaidi ya Lema.

Na hata report ya uchunguzi wa mgogoro wa madiwani wa Arusha ambao waliokuja kuchunguza alikuwa ni Dr Kitila Mkumbo na Advocate Mabere Marando pamoja na Ester iliwafikia madiwani wa chadema hata kabla ya kufikishwa kamati kuu na ndio maana madiwani wale pamoja na mimi tulikuwa tukilalamika kuna baadhi ya pages ambazo zimenyofolewa zilizokuwa zikionyesha hakuna rushwa yeyote madiwani waliyokutwa nayo. Lakini hii ni kutokana na kupata report kabla ya kuifikisha kwa kikao kilichoazimia kuunda kamati ya kuitafuta na kuiwasilisha.

Hivyo basi pasipo kuwa na kumumunya maneno ni kwamba msaliti namba moja ndani ya Chadema ni Zitto Zuberi Kabwe na hapa hawezi kupinga ukufuatilia kwenye thread niliyoandika na kufuatilia utetezi wake utaona jinsi ambavyo ndio yeye amekuwa akiwafadhili viajana hawa wasaliti ( masalia) kwa kwa kujikita kueneza propaganda za zinazotolewa na ccm za UDINI, UKABILA na UKANDA.

Rai yangu kwako bwana Zitto ni kwamba CHADEMA ni chama kinachopigania HAKI, USAWA na UKWELI, hivyo basi nakusihi urudi katika mstari ulionyooka na uungane na wapigania USAWA wenzako na uachane na njama zote za USALITI.

Na kwa tahadhari tu ni kwamba mimi tayari najihesabu TAYARI NIMESHAKUFA. Hivyo basi vitisho vyote mnavyonitumia ni kwamba haviniogopeshi hata kidogo maana katika kupigania UKWELI na HAKI najua lazima kuna kufa na mimi sintokuwa wa kwanza so niko tayari kufa bro!

Nawasilisha.

No comments:

Post a Comment

sikiliza ngoma zinazo kamata kwa sasa

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...