Sunday, November 18, 2012

Wakamatwa na noti bandia za Sh3 milioni



“Watu hao walikamatwa kutokana na ushirikiano wa polisi na raia wema kwani  ilibainika kukithiri kwa tabia hiyo hasa  wakati wa kununua mifugo kwenye minada mkoani humo,” alisema Kamanda Mpwapwa


WATU wanne ambao ni wafanyabiashara wa ng’ombe wanashikiliwa na polisi mkoani Manyara wakidaiwa kukutwa na noti bandia zenye thamani ya zaidi ya Sh3 milioni walizokuwa wanazinunulia mifugo hiyo mkoani humo.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi mkoani Manyara, Kamishna Msaidizi Akili Mpwapwa,tukio hilo lilitokea juzi wilayani Hanang’ kwenye mnada wa kununulia ng’ombe ambapo watu hao walikamatwa wakati wakinunua mifugo hiyo.
Kamanda Mpwapwa aliwataja watu hao kuwa wote ni wakazi wa wilayani Mbulu mkoani Manyara.
Alisema watu hao ambao ni wafanyabiashara wa mifugo walikuwa wananunua ng’ombe wanne kwa wafanyabiashara watatu ambao ni Detugwa Makotw (43),Jumanne Sesha (75) na John Gemahi (52).
Alisema watu hao walinunua ng’ombe wanne kwa wafugaji hao na kutoa noti za bandia kiasi  cha Sh1.9 milioni zilizokuwa kwenye noti za Sh10,000 ambapo walikutwa pia na noti nyingine za bandia sawa na Sh1.7 milioni.
“Watu hao walikamatwa kutokana na ushirikiano wa polisi na raia wema kwani  ilibainika kukithiri kwa tabia hiyo hasa  wakati wa kununua mifugo kwenye minada mkoani humo,” alisema Kamanda Mpwapwa.
Kwa upande wake, Mkuu wa upelelezi na makosa ya jinai mkoani Manyara, Benedict Msuya alisema wamefanikisha kukamata wafanyabiashara hao ambao walikithiri na tabia hiyo ya kununua mifugo kwa kutumia noti bandia.
Msuya alitoa wito kwa wakazi wa mkoa huo kuwa na tahadhari pindi wanapokuwa wauza au kununua mifugo au bidhaa nyingine za thamani kwa kuchunguza noti hizo za bandia. 

No comments:

Post a Comment

sikiliza ngoma zinazo kamata kwa sasa

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...